LYRIC

[ Chorus ] Usiku wa leo masela tupo ndani ya party
Wote tunaruka tunadance na ma shawty (eeh) (eeh)
Eeh eeeh wote tumebling (eeh) (eeh)
Dance kwenye flow and dancing ohhh
Kata kati (ooh)
Please weka mikono hewaaani
(eeh) (eeeh)

[ verse 1. Structure P ] Usiku wa leo ndani ya party si
Mchezo
Pilipili kibao lazima kuna mauzo
Hapo nimekubali kwa wengi itakuwa gumzo
Hey Mr. Dj embu shusha mijazo
Iliyokwenda shule kwetu iwe ni funzo
Ruka ruka dance tufurahi kwa pamoja Sijaona mi sababu ya we kungoja
Embu nipe raha
Nijidai
Nifurahi
Ikiwezekana basi wote tujidai
Hii nafasi yangu mimi mwenyewe tu
Na sintomind kuona hapo mtu
Mum nipe raha tushangaze hawa watu
Cheki masister du ndani ya bli walivyoshine
Hapa hakuna juice watoto wote ni wine
Simu zote mezani hakuna kwenda hewani
Waliovaa kanga naomba watupe chini
Hili ni night party na hatupo msibani
Embu mcheki sister mwenye kitopu
White
Kweli nimekubali anakwenda na wakati
Amekatika kati mpaka kashusha sketi
Mwanadamu hamu sina hamu wafahamu
Najiepusha sana na matendo haramu, Chunga sana mah hapa kuna HIV
We ukichoka basi macho kwenye tv au ushike MIC
Kuliko ule raha na wale ma vip
Heri tu uje tubanane na mimi Structure P

[ Chorus ] Usiku wa leo masela tupo ndani ya party
Wote tunaruka tunadance na ma-shawty (eeh) (eeh)
Eeh eeeh wote tumebling eeh eeh
Dance kwenye flow and dancing (ohhh)
Kata kati (ooh)
Please weka mikono hewaaani,
(Eeh) (eeeh)

[ Verse 2. Mr Puaz ] Pata taswira kali pitia yangu
Mashairi
Muda mfupi ujao utapata jibu kamili
Hutakiwi kuwa lonely ukajapigwa magoli
No time to waste fungua yako akili
Tafuta zako pene kisha nyingi uzichange
Jiweke sop kimwili kila upande
Andaa zako bling upite wakuite king
Na masister duu mapozi waitwe queen
(Yeah)
Uzivae zikukae fresh kwako mwilini
Piga full white simu sikioni una chat
Muda ukifika usiku wa leo upo fiti
Tujidai tufurahi milupo kwanza baadae
Acha babaika kacheze na umpendae Hapa Nizo B utanikuta niko bling

[ Verse 3. Eddy G ] Hapa bling bling toka juu mpaka chini
Kwa monekano hii party itakuwa makini
Masister duu mabrother men ndo usiseme
Yani usiku wa leo upo full usipime
Kwenye sekta ya vinywaji eeh bana kila kitu ni shwari
Kila kitu kipo yani mpaka pombe kali
Wapenda ulabu sekta yenu haina tabu
Ukikosa babu yani itakuwa aibu
Bora uwahi kuna muda wa dinner
Yani usiku wa leo usikose fanya hima
Ni part ya kistaarbu ya kupata
Ulabu
Ni eddy G usiku wa leo nipo Club

Hatiyani kurupushani zako
Sasa nimekubali na nimevuta picha karibu mfasili
Nimemix sana misemo na methali
Kweli hili ni bonge la party si mchezo
Watu wanavyoshake embu mcheki Nizo
Hivi hujaamini kama kweli hili gumzo
Basi nipe raha nile raha kwa furaha isijekuwa bala mwishoni
Ikawa karaha
Hivi ni nini unachotathmini
Kichwani akilini
Panda jukwaani utupe tafrani makini kwa yakini
Walakini no mi nasema no,
Au kama unabisha embu sikia michano
Leta migongano wala si malumbano
Hili ni fataki kimantiki (maah)
Ndo mana sishikiki sitamaniki (mah)

Added by

Admin

SHARE

Your email address will not be published. Required fields are marked *

ADVERTISEMENT